Kwa wiki kadhaa vyanzo mbalimbali vya habari vimekuwa vikitoa dondoo kwa yale ambayo yatatotea kwenye maonyesho ya Google I/O 2021 na hatimae shughuli hiyo imemalizika vyema leo huku vile fununu fununu ya kipi kitatoka zimekwisha.
Kabla ya kwenda mbali ni vyema ukafahamu Google I/O ni nini. Haya ni maonyesho ya kila mwaka mabayo yanaandaliwa kila mwaka na waundaji wa vitu mbalimbali wanakutana na kuonyesha kilichoboreshwa, kinachokuja kwa vitu vinavyohusina na Google. Mwaka 2021 maonyesho hayo yamefanyika kuanzia Mei 18-20.
Vitu vilivyoonekana kwenye Google I/O 2021
Android 12 Beta. Wakati wa maonyesho hayo mefahamika kinagaubaga kwamba Android 12 sasa imefikia hatua ya majaribio ya ndani kwa ndani na baadhi ya watu wachache sana. Hata hivyo, muonekano wa toleo hilo la Android 12 ulioweza kuonekana japo kwa vipengele vichache.
Kufuta kitu kwa haraka+Usalama. Katika maonyesho hayo Google wamenyesha jinsi ambavyo kivinjari chake kimeboreshwa ambapo mtu ana uwezo wa kufuta tovuti alizotembelea ndani ya dakika 15 zilizopita. Halikadhalika, uwezo wa kuweka nenosiri kisanduku utakachokitengenza ndani ya Google Photos; anayemiliki ndio ana uwezo wa kuona kilichopo ndani na wala hazitaonekana kwenye ukurasa wa picha au kweye zile ambazo umezisambaza kwa wengine.
Uwezo wa kubadili nywila kwa haraka. Kuna namna ambavyo Google imefanya maboresho na kukupa taarifa iwapo nenosiri lako si salama tena tena hivyo inakupasa kubadili haraka iwezekanavyo.
Uwanja mpana wa kuapta majibu. Google inafanyia kazi mpango wa kuongeza kuleta majibu ya ziada iwapo mtu atatafuta kitu. Mfano unapiga picha ya vitu fulani kisha unauliza mfumo iwapo vinafaa kupanda milima ya Uluguru na kutoa majibu baada ya kuipisha picha husika kwenye mfumo wao.
Ujio wa programu tumishi npya. Katika siku za usoni watumiaji wa simu za Android wataletewa programu tumishi mpya ambapo mtumiaji ataweza kubadilisha simu janja na kuwa kitenzambali (kifaa cha kubadilisha chaneli kwenye runinga) kutumia kwenye runinga janja za Android. Vilevile, kwenye magari pia mfumo wa Android unaboreshwa; inaelezwa kuna baadhi ya magari yanaruhusu kutumia simu janja ya Android kama ufunguo wa kuwasha gari.
Google WearOS na Tizen kuwa kitu kimoja. Google na Samsung waunganisha nguvu kuhakikisha programu zao enedshi kwa ajili ya saa janja (Google-WearOS na Samsung-Tizen) ambapo katika ushirikano huo waundaji watatengeneza programu tumishi na hata kuxiweka kwenye Playstore ambazo zitaweza kutumika pande zote mbili.
Mawasiliano kwa njia ya picha jongefu kuwa na uhalisia. Google wanafanyia kazi namna ya kufanya mawasiliano kwa njia ya picha mnato kuwa na uhalisia ndani yake; mfano ukimpigia mtu basi nusu uonekane wewe na nusu nyingine aonekane yule uliyempigia.
Mengineyo
Tukiangazia kwa haraqka haraka ambayo Google inaboresha ni:
- Teknolojia ya AR na matumizi yake kwenye simu janja za Android,
- Kukumbuka sehemu ambazo umeshazitembelea kwa kutumia Google Map,
- Fitbit kufanya kazi kwenye WearOS.
Ama kwa hakika zilikuwa ni siku tatu zenye mengi ambapo watu wameweza kufahamu vitu mbalimbali vinavyohusiana na Google. Kazi yetu sisi ni kukuhabarisha hivyo basi usisite kutembelea tovuti yetu kila inapoitwa leo ili kuweza kufahamu mengi.
Vyanzo: ZDNet, GSMArena
No Comment! Be the first one.