Serikali ya Kenya inatathmini kudhibiti matumizi ya WhatsApp na Skype katika hatua ambayo inaweza kulazimisha wamiliki wa huduma hizo kutoa habari kwa serikali.
Mamlaka ya Mawasiliano Kenya inatafuta mkandarasi wa kuchunguza na kuamua jinsi huduma hizo zinaweza kudhibitiwa. Mamlaka hiyo inataka kuwa na uwezo wa kudhibiti kama inavyofanya mawasiliano ya simu ya kampuni za mawasiliano ya kawaida.
Wenye mamlaka wamesukumwa kufikiria kuchukua hatua hiyo kutokana na kwamba kampuni hizo kuwa na uwezo wa kupata habari za wateja wao lakini hawana ofisi nchini Kenya.
Sheria hizo pia zitajumuishwa kuhusiana na jinsi huduma hizo zitatolewa kuambatana na mahitaji ya mashirika ya usalama kuhusiana na utoaji wa data kama zinavyofanya kampuni kama vile Safaricom inapoagizwa na mahakama.
Chanzo lazima kiwepo.
Uwepo wa WhatsApp umepunguza sana matumizi ya kupiga simu/kutuma ujumbe mfupi wa maandishi; lwa takwimu za mamlaka husika nchini Kenya wastani wa jumbe 96.3 katika kipindi cha Januari-Machi 2018 kutoka jumbe 156.8 kwa wastani katika kipindi cha miezi mitatu mpaka kufikia mwezi Septemba 2017.