Kila mwaka imekuwa kama desturi kwa Apple kufanya uzinduzi mkubwa wa bidhaa zao na baada ya muuda kidogo kuingia sokoni. Sasa ni rasmi kuwa “iPhone za Septemba” mwaka huu zitachelewa kuingia sokoni.
Moja ya bidhaa ambazo zinatazamiwa kutoka mwezi Septemba 2020 ni iPhone 12 ambapo kwa miezi kadhaa mengi ya chini kwa chini yameweza kufahamika na pengine kuweza kuingia sokoni muda mchache baada ya uzinduzi lakini mambo si hivyo kama ilivyokuwa ikitarajiwa.
Kwa mujibu wa The Wall Street Journey, mapema mwaka huu waliliripoti kuwa Apple watachelewesha utengenezaji wa kiwango cha juu angalau kwa mwezi mmoja hivi.
Utakumbuka Apple walitoa iPhone 8 na X kwa pamoja zilitoka mwaka 2017 lakini zikaingia sokoni mwezi Oktoba. Hivyo hivyo kwa iPhone XR iliyotoka mwaka 2018 na kupelekwa sokoni mwezi Oktoba ya mwaka huo kutokana na kuwepo na matatizo ya vioo vya LCD vilivyotumika kwenye bidhaa hizo.
Suala hilo litaathiri mauzo ya bidhaa za Apple kwa robo ya tatu na mbali na hilo Qualcomm pia wameongelea suala kama hilo ambao pia wana mkono wao kwenye bidhaa za Apple.
Vyanzo: The Verge, GSMArena, Gadgets 360
2 Comments
Comments are closed.