Kuna kampuni 4 za ving’amuzi Tanzania zinazohusika na utoaji wa huduma ya taarifa mbalimbali kupitia runinga. Taarifa hizi zinazotolewa kupitia ving’amuzi ni pamoja na taarifa za kuelimisha, kuburudisha na kusisimua.
Mamlaka ya mawasiliano nchini Tanzania TCRA inahusika na usajili wa hivi vingamuzi kwaajili ya kutoa huduma kwa watanzania. Vituo vyote vya televisheni vinavyopatikana nchini huonyeshwa kwenye ving’amuzi hivi ikiwemo TBC 1, Channel Ten, ITV, EATV na StarTV. Kampuni hizo za ving’amuzi zilizopo Tanzania ni:
Dstv: Ni kampuni ya king’amuzi inayoonyesha taarifa mbalimbali kutoka katika vituo vya habari vya ndani na nje ya nchi. Kampuni hii inatokea Afrika ya kusini na imejihusisha na utoaji wa huduma hii kwa nchi zilizo kusini mwa jangwa la sahara. Baadhi ya chaneli maarufu zinazopatikana Dstv ni kama Supersports na National Geographic.
AzamTv: Ni kampuni ya king’amuzi inayotoa huduma zake kwa nchi za Afrika mashariki. Kampuni hii imefanikiwa kuweza kuonyesha mbashara wa mechi za mpira wa miguu zinazochezwa nchini na hii imeipa sifa sana na kupelekea watu kununua king’amuzi na kutumia huduma zao.
Startimes: Kampuni hii inamilikiwa na wachina na inatoa huduma za kuonyesha taarifa mbalimbali kutoka katika vituo vya televisheni vya nchini na vya nchi za nje. Baadhi ya chaneli zinazoonyeshwa katika king’amuzi hiki ni MamboTv, Nevela.
Zuku: Hii ni kampuni ya kimataifa inayotoa huduma za mtandao pamoja na huduma za televisheni. Huduma za kampuni hii zinapatikana kwenye nchi zote za Afrika mashariki.
No Comment! Be the first one.