Wengi tumewahi kusikia neno Alibaba lakini wachache wanaofahamu kuwa Alibaba ni nini. Alibaba ni soko la kibiashara mtandaoni ambalo wauzaji na wanunuaji kutoka sehemu mbalimbali duniani hukutana na kufanya biashara.
Kampuni hii ya Alibaba ilianzishwa mwaka 1999 na mmiliki wake Jack Ma. Kipindi inaanzishwa kampuni hii ilikuwa inatoa huduma moja tu kupitia tovuti yake ya Alibaba.com. Tovuti hii ilisaidia kuunganisha wauzaji wa bidhaa za kwenda nchi za nje waliopo nchini China pamoja na nchi nyingine na makampuni katika nchi zaidi ya 190.
Wasambazaji wa bidhaa hutumia tovuti ya alibaba kuuza malighafi au bidhaa zao za viwandani. Pia wanunuaji ni wale watu wanaonunua bidhaa rejareja au wauzaji bidhaa za jumla. Kuna sababu nyingi zinazoweza kupelekea mtu kununulia bidhaa zake alibaba ikiwemo unafuu wa bei, urahisi wa kutumia pamoja na wingi wa bidhaa za kuchagua.
Tangu kuanzishwa kwake kampuni hii imekuwa ikikua na hii imepelekea kuongeza huduma zingine kama Alipay, Alimama, Taobao, Tmall, Freshipo, AliExpres, Lazada, Ding talk na zingine nyingi.
No Comment! Be the first one.