Pale vifaa vyetu vinavyokuwa vimeishiwa na bando (MB/GB) WiFi huwa ndio kimbilio letu. WiFi hii ndio hutuwezesha kufanya mambo mbalimbali katika vifaa vyetu kwa kutumia huduma ya intaneti
Kuna wengine WiFi wanazo majumbani kwao, wanazitumia kwa matumizi madogo madogo ya kifamilia, wengine zipo katika maofi. Na zingine zipo tuu mitaani.
WiFi hizi unaweza ukashangaa zinatumiwa na watu wengi sana mara moja na kwa pamoja. Hii inaweza ikazisababisha zikawa na spidi ndogo.
Je ni mambo gani unaweza kufanya ili kufanya Spidi ya intaneti ya WiFi ikaongezeka?
1. Weka Router (Inayosambaza WiFi) katika Eneo Sahihi
Router zote inabidi zisifichwe kamwe, inabidi ziwekwe kwenye eneo la uwazi ambapo hakuna vitu ambavyo kwa namna moja au nyinigne vitasababisha network isiwe nzuri kama vile ukuta n.k
Ili kuwa na uhakika kabisa ‘Router’ hiyo inabidi ikae katika eneo la uwazi kabisa na ikiwezekana ikae kati kati ya nyumba ili kuwezesha kila mtu kuweza kupata network kwa urahisi
2. Zuia Muingiliano Wa Ki ‘Network’
Vifaa kama vile vile vya kuangalia watoto wanafanya nini (baby Monitors), simu na hata majiko ya umeme ya uokaji (microwave ovens) vinaweza vikasababisha WiFi yako ikawa inazingua katika swala zima la network. Kuondoa ile Router na kuipeleka mbali kidogo na vifaa hivyo inaweza ikasaidia pia
3. Imarisha Ulinzi
Unaweza ukashangaa tuu intaneti ya WiFi yako imekua finyu tuu lakini ukichunguza vizuri unagundua kuwa sio nyie tuu (wanafamilia) mnaoitumia, bali kuna watu wengi kama vile majirani n.k. Hali hii pekee inaweza sababisha intaneti ikawa chini. Ili kuhakikisha kuwa hili halijitokezi basi huna budi kuweka ulinzi kwa kuweka vitu kama NenoSiri (Password) na vile vile usiweke wazi neno siri hili kwa watu ambao hawahusiki na WiFi hiyo
4. Zuia Apps/Vitu Ambazo Zinakula Data Kwa Kiasi Kikubwa
Kuna vitu vinakula data sana vitu kama vile kuangalia video katika mtandao na kusikiliza muziki. Ukiachana na kuangalia mafaili ya video mbalimbali ambao yana ubora wa HD unaweza ukashangaa katika familia kuna mtu anatumia intaneti hiyo katika kushusha (Download) mafaili makubwa kabisa. Vitu kama hivyo inabidi vifanyike wakati hakuna mtu mwingine ambae anatumia WiFi hiyo na nyakati bora ni za usiku
Kama WiFi yako ilikuwa inasuasua mpaka hapo nadhani utakua umeshaipatia dawa. Niandikie sehemu ya comment hili wewe umelipokea vipi? Ningependa kusikia kutoka kwako