Idadi ya watumiaji wa intaneti duniani imezidi kuongezeka na huku bara la Afrika likishika nafasi ya tatu kwa wingi wa watumiaji.
Idadi ya watu wanaotumia intaneti ulimwenguni, kufikia Julai mwaka huu imefikia watu bilioni 4.4, huu ni ukuaji mkubwa kutoka watumiaji bilioni 3 Julai mwaka jana.
Hayo ni kulingana na taarifa iliyojumuishwa kutoka katika ripoti ya mtandao wa DataReportal iliyochapishwa kuhusiana na idadi ya watumiaji wa Intaneti inayoendelea kuongezeka ulimwenguni.
Kanda ya Asia Mashariki ni ya kwanza na watumiaji wa Intaneti wanaofikia bilioni 1, wakati eneo la Asia Mashariki na Asia Kusini likiwa na watumiaji milioni 803.
China inafuatwa na India ikiwa na watumiaji milioni 560 na Marekani ikiwa na milioni 292. Singapore inafuatiwa na Hong Kong na kisha Korea Kusini.
Tanzania imekuwa miongoni mwa nchi tatu za juu Afrika ambazo idadi ya watumiaji wa intaneti inakua kwa kasi kubwa, hii ikiwa nyuma ya Sahara Magharibi na Djibouti.
Tanzania inakadiriwa kuwa na watumiaji zaidi ya milioni 14.5 kulingana na data za kimataifa.
Bara la Asia kwa ujumla wake lina watumiaji zaidi ya bilioni 2.2, huku bara la Ulaya likifuatia likiwa na watumiaji milioni 719. Bara la Afrika lina watumiaji milioni 525.