Huawei wazidi kuporomoka kimauzo katika soko la uuzaji simu duniani. Data zinaonesha Samsung wakizidi kulishika soko huku Huawei mambo yakienda tofauti kwao.
Data za kimauzo zinlizotolewa na shirika la utafiti masoko la Counterpoint Research zinaonesha kwa mwezi Agosti mwaka huu Samsung walishika asilimia 22 ya mauzo yote ya simu janja duniani. Hii ni nafasi ya juu ukilinganisha na mwezi wa Aprili mwaka huu ambapo mauzo yao yalikuwa asilimia 20 na huku Huawei alikuwa namba moja akishika soko la simu janja kwa asilimia 21.
Kutoka ushikaji soko wa asilimia 21 mwezi wa nne, hadi asilimia 16 mwezi wa nane mwaka huu hili ni anguka la asilimia kubwa kwa Huawei na linahusishwa moja kwa moja na vikwazo vya kibiashara ambavyo imewekewa na Marekani.
Xiaomi ndio moja ya kampuni inayonufaika zaidi pia na hali hii ya Huawei ambapo nafasi yao kimauzo imepanda kutoka asilimia 8 mwezi wa nne hadi kufikia asilimia 11 mwezi wa nane. Kwa wanunuaji wengi wa simu hasa wa barani Ulaya, Xiaomi inaonekana kama ndio kampuni nyingine ya kichina inayoweza kuaminika zaidi kwenye ubora wa simu zake na huku apps za Google na soko lake vikiwa vinapatikana kwenye simu hizo.
No Comment! Be the first one.