Unakumbuka kuna kipindi Apple na Android walikaa chini na wakatengeneza App ambayo itasaidia kuhamisha vitu kama namba za simu n.k
Mwanzoni kabisa uwezo wa App hiyo ulikua ni mdogo, na ulikua unaweza kuhaimisha vitu vya muhimu muhimu –kwa haraka haraka—tuu
Sasa umeshwahi kufikiria kama unatumia WhatsApp katika kifaa cha Android lakini unataka ubadili matumizi yako ya simu na kuhamia katika simu ya iPhone.
Hapo awali ilikua ikitokea hivi hakuna namna bali ilibidi kwanza uweze kuhifadhi taarifa zako katika mtandoa (mfano, Google Drive) katika kifaa unachotumia
Baada ya hapo ilikuladhimu kwa kutumia kifaa kingine uweze kurudisha hifadhi hiyo ya mazungumzo hayo (hapa fikiria kama ulikua unatumia Android na umeenda katika iPhone).
Sasa Hivi Kwa kutumia App hiyo hiyo ya Move To iOS ambayo ilitengenezwa na Android kwa kushirikiana na Apple utaweza hamisha mazungumzo ya WhatsApp katika vifaa vyenye programu endeshi tofauti (Android na iOS)
Ni wazi kuwa watumiaji wengi wa WhatsApp ni wanatumia katika vifaa vya Android, fikiri litakua ni jambo la aina yake kuona watumiaji hao kwa wingi wakihamia na kuanza kutumia WhatsApp katika vifaa vya iOS sio?
Ili kuwezesha hili hakikisha kuwa una toleo jipya kabisa la hiyo App ya Move To iOS, vile vile kifaa cha Android kiwe kina Android Lollipop (Android 5) na iPhone iwe na iOS15.5.
Soma Kila Kitu Kuhusiana Na Move To iOS >>HAPA<<
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika uwanja wa comment, hii umeipokeaje? Je ushwahi kutumia hii App?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.