Kampuni ya Facebook imesema itafanya uchunguzi kuhusiana na suala la kudhibiti idadi ya taarifa za habari zinazochapishwa na kusomwa bila malipo kwenye mtandao huo.
Taarifa hii inakuja wakati ambapo Facebook imekuwa chanzo muhimu cha habari kwa watu wengi hali ambayo imezua malalamishi kutoka kwa wachapishaji wanaodai hupoteza fedha nyingi na udhibiti wakati habari zao zinaenezwa bure katika mtandao wa Facebook.
Kwanini udhibiti huo umeanza kuwekewa mkazo hivi sasa?
Yamekuwepo malalamiko mengi kutoka kwa wanaoandaa habari kutumia kiasi kikubwa kufanikisha taarifa kukamilika halafu mwisho wa siku chanzo cha habari kunakuwa hakifaidiki na kile kilichoandaa (habari) hivyo kupelekea Facebook kuamua kuwa wanaoweka taarifa watakuwa wakilipia baada ya kampuni hiyo inazindua mfumo wa kulipa kwanza kabla ya kuweka taarifa.
Huduma hiyo ilianzishwa miaka miwili iliyopita na inashindana na huduma ya Google ya AMP ambayo hutumia habari kutoka kwa mashirika yaliyochaguliwa na ambayo habari zake zinaweza kupatikana kwa njia ya simu.