Ni jambo lililozoeleka kuwa mtu anapopiga miayo ni ishara ya kuwa anahisi uchovu au ana njaa na wakati mwingine vyote kwa pamoja lakini katika utafiti uliofanywa na wanasayansi hivi karibuni umegundua kitu ambacho hakikufahamika huko nyuma.
Swali la “Kwanini mtu hupiga miayo?” ambapo muuliza swali angetegemea kupata jibu la kisayansi zaidi limeweza kupata majibu na TeknoKona tunaamini baada ya kumaliza kusoma makala hii utakuwa umeelimika.
Timu ya watafiti katika Chuo kikuu cha Nottingham, imegundua sehemu ya primary motor cortex (ambayo ni sehemu ya ndani ya ubongo wa binadamu) pia inatumika sehemu kubwa wakati mtu anapopatwa na ugonjwa wa neva. Kupiga miayo mara kwa mara, ni dalili ya “Echophenomena“ – yaani namna ya kuiga maneno na matendo ya mtu mwingine bila kujua.
Hali hii ya Echophenomena pia inaonekama kwa mtu anayeugua ugonjwa wa neva au mtu anayeugua kifafa na tawahudi. Katika uchunguzi wa wanasayansi watu 36 waliojitolea kufanyiwa uchunguzi na walipokuwa wanafanyiwa uchunguzi wa kisayansi wengine walipiga miayo.