Benki ya NMB na kampuni ya mawasiliano ya Halotel zimeingia mkataba wa makubaliano ya miaka miwili ya kutoa huduma za TEHAMA katika shule za serikali zaidi ya 200 hapa nchini.
Makubaliano hayo yamefanyika Agosti Mosi mbele ya waandishi wa habari na mwaka wa kwanza NMB itatoa kompyuta 350 kwa shule 100 na jukumu la Halotel litakuwa ni kuziunganisha na huduma ya intaneti.
Katika kuzipata shule hizo serikali itashirikiana na Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Wizara ya Elimu.
Mkurugenzi Mtendaji wa NMB, Bi. Ineke Bussemaker amesema kwa kushirikiana na Halotel kila shule ambayo NMB itatoa kompyuta Halotel watatoa huduma ya intaneti na mahali ambapo Halotel watataka kupeleka Intaneti NMB itatoa kompyuta.
NMB ianataka kusaidia taifa na kuwa na watu wenye weledi hususani masuala ya TEHAMA bila kuwa na watu wengi wenye weledi hata biashara haziwezi kufanyika kwani mtu akiunganishwa na intaneti anakuwa ameunganishwa na dunia.
Upande wa Kaimu Mkurugenzi wa Halotel, Nguyen Van Son amesema wao wako tayari kushirikiana na wadau wote wa maendeleo ya elimu nchini.