Xiaomi kwa sasa wana mpango wa kuja na matoleo mengi ya simu za Xiaomi 13, pengine hii ndio itakua simu yao shindani kabisa na simu zingine kwa muda wa mwaka mmoja.
Kwa fununu ambazo zinasambaa ni kwamba matoleo haya ya simu hizo yataanza kutambulishwa ndani ya mwezi novemba mwaka 2022.
Mwaka 2021 kampuni ilizindua rasmi matoleo yake ya simu za Xiaomi 12 na tuliandika kuhusiana na hilo >>HAPA<<
Ni wazi kuwa kampuni ya Xiaomi ni moja kati ya makampuni makubwa sana kwenye maswala ya kutengeneza na kuuza simu janja.
Kwa mwaka huu tuu kampuni hiyo imeshika nafasi za juu kabisa katika kampuni za simu ambazo zimefanya vizuri kwa kuuza simu janja nyingi duniani.
Kwa mujibuwa taarifa zilizotolewa na Digital Chat Station ni kwamba matoeo ya Xiaomi 13 yatakua na kamera nyingi zenye uwezo wa MP 50.
Yaani hapa kutakuwa na toleo ambalo lina kamera mbili ambazo zote zina MP50 na toleo linguine lenye kamera tatu ambazo zote zina MP50.
Matoleo ya Xiaomi 13 na Xiaomi 13 Pro yataingia kwa mara ya kwanza kabisa katika soko la simu janja huko nchini china.
Utofauti wa matoleo haya mawili ya simu janja ni kwamba utakuwa kwenye kamera ya mbele na hata aina ya lensi na pengine kutakua na toleo linguine linalojulikana kama Xiaomi 13 Ultra.
Xiaomi 13 Ultra ni kwamba litakaa na kamera nzuri zaidi na uwezo mkubwa sana katika lensi zake. Kampuni ikizindua simu hizo mwezi novemba ndipo kila kitu kitakua sawa sio?
Ningependa kusikia kutoka kwako, naindikie hapo chini katika eneo la comment, je unadhani simu hii ikitoka itakua ni mshindani mkubwa kwa simu janja zinazotegemewa kutoka mwaka huu?
Kumbuka Kutembelea Mtandaoa Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.