Apple TV+ ni huduma kama ilivyo mtandao wa Netflix lakini kikubwa ni kwamba huduma hiyo inapatikana katika vifaa vingi vya Apple.
Tuliandika kuhusiana na kampuni ya Netflix kupoteza wateja, unaweza kusoma zaidi >>HAPA<< Kabla hatujaendelea na Apple TV+
Ukiachana na hayo kwa sasa inaonyesha kuwa kampuni ya Apple kupitia Apple TV+ imejionea wateja wanaotumia huduma hiyo kuongezeka zaidi.
Hii kwa namna moja au nyingine inaonyesha ukuaji wa huduma hiyo huku ukiangalia huduma zingine kama hii zinasua sua katika swala zima la ukuaji.
Kumbuka pia katika huduma hiyo ya Apple huwa kuna maonyesho ambayo yanapatikana katika mtandao huo tuu
Yaani kwa maana nyingine ni kwamba huwezi kuyapata pengine popote, pengine uzuri wa maonyesho (filamu, tamthilia n.k) ndio unafanya wateja wengi kujiunga na huduma hiyo.
Kumbuka mitandao kama Netflix na Disney+ ukiachana na kuhangaika tuu katika kupata wateja wapya na kuwabakiza wale ambao wanao kwa sasa.
Kampuni ya Netflix tuu imekuja na baadhi ya vifurushi vya gharama ya chini lakini vikiwa vimeambatana na matangazo mbalimbali ambayo yatakua yanatangaza biashara au bidhaa mbalimbali.
Ni wazi kuwa makampuni ya kiteknolojia mengi yanapitia katika wakati mgumu sana katika kuhakikisha kuwa wanapata mapato ya kutosha, isitoshe kuna janga la kuporomoka kwa uchumi
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika eneo la comment, je umeshawahi kutumia huduma hii? Niambia uzoefu wako na huduma hii!
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.