Baada ya miezi ya kadhaa ya tetesi hatimaye wamiliki wa app ya WhatsApp wamezindua huduma ya malipo ya kutuma pesa kutoka kwa mtumiaji mmoja mpaka mwingine kwa nchi ya Brazil.
Huduma hiyo imeanza rasmi masaa machache yaliyopita kwa nchi hiyo yenye watumia wa WhatsApp takribani
milioni 120. Huduma hiyo itakuwa inapatikana bila ya kumuathiri mtumiaji kwenye matumizi yake ya mengine ya mawasiliano.
Mfumo huo wa utumaji pesa umeunganishwa na ule wa Facebook pay ulioanza mwaka mmoja uliopita. Aidha kwa watumiaji wa iOS wataunganishwa na Messages app.
Ili mtumiaji aweze kutuma au kupokea pesa atalazimika kuunganisha akaunti yake ya
WhatsApp na kadi yake ya Benki aidha ya Visa Card, Mastercard au Debit card.
Hata hivyo huduma hii kuanza nchini Brazil imewashangaza wengi badala ya nchi ya India ambayo kwa miezi kadhaa WhatsApp imekuwa kwenye majaribio ya huduma ya malipo kupitia Unified Payments Interface(UPI).
Aidha huduma hii itawafurahisha wengi kwa kuwa watumiaji wa WhatsApp wamekuwa wakifanya biashara ya bidhaa kadhaa kupitia Programu hiyo na kulazimika kutumia njia zingine za malipo. Lakini sasa yote yatamalizwa kupitia hapo hapo WhatsApp.