Wiki iliyopita mtandao wa kijamii wa Twitter ulifungia akaunti za watumiaji kimakosa na hii ni kutokana na watu kupinga uwepo wa sera mpya ya Twitter ya kupiga marufuku usambazaji wa picha bila ridhaa ya mhusika. Miongoni mwa watu waliofungiwa akaunti zao na Twitter kimakosa ni waandishi wa habari 12 pamoja na wanaharakati wa kisiasa.
Kampuni hiyo ilisema kuwa tayari ilikuwa ikibadilisha utendaji wa sera hiyo na imeanza ukaguzi wa ndani ili kuhakikisha kuwa sera hiyo inatumika “kama ilivyokusudiwa.” Data zaidi juu ya wingi wa mashtaka ya uwongo itakuja baadaye. Sheria hiyo inazuia watumiaji kusambaza picha na video bila ruhusa ya mhusika. Pia inakataza watu kutishia kusambaza maudhui hayo au kuwachochea wengine kuyavujisha.
Ebay nayo imethibitisha kuwa ilisimamisha “idadi ndogo” ya watumiaji kimakosa mnamo tarehe 3 Desemba. Kampuni haikutoa sababu au kufichua ukubwa wa tatizo, lakini ilisema ilikuwa imerekebisha utelezi na kuwaarifu walioathirika.
Ingawa haijulikani kila mara ni nini husababisha usimamishaji wa akaunti za watumiaji kimakosa, matukio kama haya yanaonyesha mipaka ya kudhibiti huduma za mtandao. Kampuni mara nyingi hulazimika kuegemea udhibiti wa kiotomatiki ili kushughulikia kiwango kikubwa cha maudhui, na wasimamizi hao wa kibinadamu ambao wanatumika bado wanaweza kufanya makosa. Vikwazo kama hivi ni nadra, lakini inaweza kuwa vigumu kuepukika bila maamuzi ya kukagua mara mbili.
Chanzo: Engadget(Twitter) na Engadget (Ebay).
No Comment! Be the first one.