Kuna tetesi ya kwamba kampuni ya Sony ipo njiani kuja na simu yenye display ya kukunjwa. Tetesi hizo zinasema kwa sasa Sony wapo katika hatua za kutengeneza simu za mfano (prototypes) za kuweza kutambulishwa ifikapo Disemba mwaka huu.
Hii si mara ya kwanza kwa taarifa kama hizi kuja. Ila kwa sasa hivi taarifa zimekuja zikiwa na mambo mengi yanayohusiana na simu hiyo.
Display/Kioo cha simu hiyo kinatengenezwa na kampuni ya LG – ambao tayari ni watengenezaji nguli pia katika teknolojia za display/vioo vya kielektroniki.
Teknolojia ya display itakayotumika itakuwa na uwezo wa kuvutwa na kuhifadhiwa katika hali mkunjo. Kwa kifupi Sony wanataka kutengeneza simu muundo wa kitofauti zaidi ukilinganisha na simu za display ya mkunjo kutoka Samsung – Fold, Huawei na Xiaomi.
Baadhi ya sifa zilizovuja;
- Kuna optical zoom 10x
- Betri la mAh 3220
- Prosesa ya Snapdragon 855
- Uwezo wa 5G
Watafiti wengi wanaamini simu hiyo haipo njiani kuja muda wowote wa karibu. Tuliona jinsi Samsung walivyorudi tena kiwandani kuboresha simu yao ya Samsung Galaxy Fold baada ya simu kadhaa kuharibika baada ya kutumika kwa muda mfupi tuu na waandishi wa habari.
Je unadhani kuna umuhimu wa kuja na simu zenye display zinazoweza kukunjwa au unaona teknolojia ya sasa inatosha na zingebaki hivi hivi?
Vyanzo: Techradar na tovuti mbalimbali