Unakubaliana na mimi kwamba WhatsApp ni bure kutumia wala hatulipii, lakini ukweli ni kwamba WhatsApp ina sheria na masharti ambayo ukienda kinyume unaweza kufungiwa. Tutazungumzia mambo matano ambayo hupaswi kuyafanya kwenye WhatsApp, ukifanya mara kwa mara au hata mara moja tu utasababisha WhatsApp yako kufungiwa.
WhatsApp ina uwezo wa kufuta kabisa au kuifungia kwa mda akaunti yako, adhabu inategemea na kosa ulilofanya, hautokuwa na uwezo wa kutumia namba yako kwenye WhatsApp kama wakifuta akaunti yako.
VITENDO 5 VINAVYOWEZA KUFANYA AKAUNTI YAKO KUFUNGIWA.
- Epuka kutuma au kutumia maudhui yenye hatimiliki (copyright) au maudhui ya wizi (pirated).
Huenda hujui lakini WhatsApp imerekebisha sera zake ili kushughulikia maudhui ya dijitali (digital contents) yaliyoibiwa, maudhui ya Filamu, mziki na mengineyo ambayo yanaweza kutumwa kupitia WhatsApp. Ni marufuku kutuma Filamu (movies kwenye WhatsApp) ambayo ina hatimiki wengine wamekutana na changamoto ya kufungiwa akaunti zao.
WhatsApp wana mfumo ambao unaweza kugundua kama umetuma au umetumia kitu chenye hatimiliki.
2. Kuwa na tahadhari unapotumia picha kwenye WhatsApp.
Kuna baadhi ya picha ambazo haziendani na sheria na kanuni za WhatsApp, pindi unapozitumia utakuwa umeenda kinyume na sheria hizo. picha zinazoonesha ubaguzi wa rangi, kuwatenga bidamu kama Albino n.k na picha za ngono, hata kama picha zinatumika lakini ni kinyume na kanuni za WhatsApp na si kila akaunti inayotumia maudhui haya hufungiwa, akaunti baadhi tu hufungiwa sasa usiwe mmoja wa hawa wachache kufungiwa akaunti yako.
3. Epuka kutumia matoleo mengine ya WhatsApp.
Hasa kwa watumiaji wa Android wao wana uwezo wa kupakua (download) na kutumia matoleo yasiyoidhinishwa na WhatsApp (unauthorized versions of WhatsApp). haya matoleo huongezewa vipengele (features) ambavyo havipo katika toleo la msingi (default version). haya matoleo hayaruhusiwi.
Hii ndiyo sababu kubwa inayoongoza kwa kuzifanya akaunti kufungiwa, programu hizo ni kama WhatsApp Plus, Whatsapp GP n.k akaunti yako inaweza kuzuiliwa na mda kuzuiliwa moja kwa moja kutokana na kosa hilo.
4. Epuka kuripotiwa mara kwa mara.
Watumiaji wanaweza kukasirika endapo utatumia maudhui ambayo hawapendezeshwi nayo, wanaweza kukuripoti au kuizuia akaunti yako (block). ikiwa akaunti yako imeripotiwa WhatsApp inaweza kuzifikia jumbe 5 ili kuona na kupima kama ni kweli kuna kosa limefanyika. Akaunti yako inaweza kufungiwa kama itabainika kweli ulifanya makosa. kama hautolidhika na maamuzi una nafasi ya kuomba kufunguliwa akaunti yako.
5. Kutuma jumbe nyingi zinazojirudia ama kujaribu kumdukua (hacking) mtu.
Mtumiaji anapotuma jumbe/ujumbe kwa watu wengi kwa lengo la kutangaza bidhaa au jambo flani, huenda hii ikaleta kero kwa mtumiaji/watumiaji. WhatsApp imeweka kikomo cha kutuma jumbe kupitia kipengele cha share ambapo mwisho ni watu watano. mbali na hivyo unaruhusiwa kuweka ujumbe wako kwenye WhatsApp status ili watu waone au unaweza kutengeneza group ili uwatumie watu wengi kuliko kumtumia mtu mmoja mmoja kwenye orodha ya majina uliyonayo ukiendelea utaonekana kama mpotoshaji (spam account). Hii inaweza kupelekea akauti yako kufungiwa.
Kuna wengine ambao hutuma Links zenye virusi (malware) na wengine hutuma jumbe za kuonyesha ni wafanyakazi wa shirika la Meta kwa lengo la kutaka kuiba au kudukua akaunti za watu hatua hii ya kuingia usalama na faragha za watu inaweza kufanya akaunti yako ikafungiwa moja kwa moja.
Kuwa makini pindi uwapo mtandaoni au pindi utumiapo WhatsApp, ili kujiweka salama unaweza kutumia njia za kujilinda kama two-step authentication ambayo hulazimu kupata namba za kudhibitisha kabla ya kuingia kwenye akaunti yako, pili usifungue links ambazo zimetoka kwa mtu usiyemfahamu akikutaka kudhibitisha au kujisajili mahala flani. Unaweza kuripoti au kuizuia(block) namba ambayo unaona inasumbua kwa kutuma jumbe zisizokufaa.
No Comment! Be the first one.