Vita ya kibiashara iliyoanzishwa na rais wa Marekani imesababisha Uchina kufikiria namna ya kupunguza kutegemea bidhaa za zinazotengenezwa kutoka kwenye taifa linaloongoza kiuchumi.
Uchina sasa imeamua kujifunga mkanda na kuamua kutengeneza vipuri ambavyo mizizi yake ni kutoka kwa AMD (processor) za 32 Bit ambazo zitafamika kama Dhyana.
AMD haiwatengenezei Uchina kisha kuwauzia baliimewaruhusu kutengeneza za vipuri hivyo vinavyotumika kwenye kompyuta kulingana na mahitaji ya nchi yao.
Dhyana-Kipuri kilichotengenezwa na Uchina kulingana na mahitaji yao ya kitu hicho kwenye kompyuta.
Mwaka 2015, Marekani ilizuia Intel pamoja na makampuni mengine yanayotengeneza vipuri vya kwenye kompyuta kwa sababu ya kuamini vitu hivyo vilikuwa vinachagiza Uchina katika utengenezaji wa silaha hatarishi sana (nuclear).
Wezesha bando kwa kutuma kiasi chochote kupitia Selcom, kwenye simu yako bofya *150*50*1# kwenye namba ya malipo weka 60751369 jina litakuja TEKNOKONA.
Ni Mhariri Msaidizi na mtaalamu wa mambo yanayohusu kompyuta. Pia ni mmoja wa wafuasi wakubwa katika teknolojia; Dunia ya sasa inaendeshwa kwa teknolojia.
Wasiliana nami kupitia |ericmato@teknokona.com|