VYUO VINGI VITAANZA MWAKA WA MASOMO MPYA NDANI YA KIPINDI HICHI,
KWA WANAOANZA CHUO NA WANAOTAKA FANYA MANUNUZI MAPYA..
Kuna watu watakaonunua laptop kwa mara ya kwanza, kuna mtu mwingine atataka kufanya mabadiliko ya simu, pia kuna maamuzi juu ya modem za huduma ya intaneti…na kingine Je kama unaitaji tablet basi ununue ipi?
Je utanunua ipi? Tumejitahidi kuja na mwongozo rahisi wa kukusaidia katika kufanya maamuzi kulingana na mahitaji yako na bajeti yako.
LAPTOP
Je utanunua mpya au iliyotumika? Na zaidi ya hapo je uchague ipi? Samsung, HP, Dell, Toshiba au Acer?
DELL na TOSHIBA Ndiyo Zinapatikana Kwa Bei Raisi Zaidi |
Kwa kuanzia kama unampango wa kununua laptop mpya kwa asilimia kubwa ningekushauri kama una laptop nyingine basi uvumilie na kusubiri toleo la laptop zitakazokuja na Windows 8 zinazotegemewa kuingia sokoni mwisho wa mwezi wa kumi mwaka huu. Lakini pia itakuwa vizuri kwa sababu hata kama utataka kununua ya Windows 7 basi kuna uwezekano mkubwa wa laptop nyingi zinazotumia Windows Vista na 7 kushuka bei kwa kiasi kikubwa.
Laptop zinazotumia Windows 7 nyingi zinaweza kuwekwa Windows 8 na zaidi ya yote kama itakuwa Windows 7 halali na sio feki basi utaweza kuweka (upgrade to) Windows 8 kupitia intaneti kwa takribani dola 39.99 za Marekani.
Laptop Ya Toshiba |
Hivyo kama una bajeti ya kwenye milioni moja na uaweza kusubiri basi subiri uje ununue laptop zitakazokuwa zimetengenezwa kwa uwezo wa Windows 8.
Nje ya hapo unaweza tembelea tovuti ya www.inauzwa.com na kuangalia laptop zilizotumika na kununua kutoka kwa watu ambao wameweka namba zao za simu kwa uraisi zaidi, hii ni kwa sababu utaweza kukutana na mtu na kuangalia kabla ya kununua, ila kama bajeti imetulia ni bora kuingia mwenyewe madukani na kuchagua kulingana na mapendeleo yako. Kitu kizuri zaidi ni kuwa bei za laptop zimeshuka kwa sababu ya ujio wa Windows 8, hivyo huu ni wakati mzuri wa kufanya manunuzi kama hauna nia ya kununua laptop yenye Windows 8 kutoka kiwandani. Ukiwa na bajeti ya kuanzia laki 800 hadi milioni 1 na laki mbili unaweza pata laptop nzuri tuu madukani tena zikiwa mpya.
Laptop Ndogo za Acer, Maarufu Kama AspireOne ni Moja ya Laptops Nzuri Zaidi Kwa Bei Ndogo |
Kwa mtu ambaye anaitaji laptop kwa ajili ya matumizi madogo kama kuandaa taarifa na kutumia intaneti, na kuongezea hapendi mzigo basi ni bora kufanya uamuzi wa kununua Mini Laptops, ambazo ni laptop ndogo zisizokuwa na uwezo wa kutumia CD. Uzuri mwingine wa hizi ni uwezo mzuri wa kutumiwa kwenye chaji kwa muda mrefu.
Kwa laki 4 hadi tano na nusu unaweza pata nzuri toka kwa kampuni ya Acer, Samsung na HP kwa ufupi. Kwa hali ya ubora katika aina hii ya laptop nitakushauri kununua za Acer.
TABLETS
Watu wengi wameanza kuvutiwa na Tablets ingawa bado wengi hawajaelewa matumizi yake bado. Ila kwa kifupi tablet zinakusaidia kufanya kazi nyingi ambazo unaweza fanya kwa kutumia laptop/kompyuta lakini hapa asa ni kwa urahisi wa kubeba popote na pia kwa zile zinazokubali kuwekwa laini ya simu basi utaweza pata huduma za intaneti kwa urahisi zaidi popote palipo na mtandao. Kingine ni urahisi wa kubeba na kutumia katika mazingira ambayo isingekuwa rahisi wewe kubeba laptop, na zaidi ya yote tablet nyingi zina uwezo wa kukaa na chaji muda mrefu zaidi kuanzia masaa 6 hadi zaidi ya 7.
Tablet Kutoka Microsoft ya Surface Inategemewa Kuuzwa Chini ya Laki 3 na nusu. |
Bei za tablets zinatofautiana kulingana na vitu kama uwezo wa utunzaji data, uwezo wa kuweka chaji, uwezo wa huduma za intaneti kama ni kupitia laini au ‘Wireless’, na pia ‘brand’/ kampuni husika. Mfano tablets za Apple, iPads huuzwa kwa bei juu zaidi kulinganisha na za makampuni kama Blackberry Playbook, Samsung, Asus, HP, na zingine nyingi zinazotumia Android. Na habari nzuri zaidi kampuni ya Microsoft nayo ipo njiani kuleta tablet itakayotumia Windows RT ambayo ni Windows 8 iliyotengezwa kwa ajili ya tablets itakayotambulika kama Surface, nayo tunategemea itazinduliwa hapo mwisho wa mwezi wa kumi.
iPad ni Nzuri Sana, Ila ni Ghari Zaidi iPad 3 zinauzwa Kuanzia 800,000/= |
Hivyo katika kuchagua tablets angalia bajeti yako ya fedha na pia je unaitaji tablet kwa kazi gani hasa. Tablets nzuri zinapatikana kuanzia dola za kimarekani 199 (takribani Tsh 320,000/=) mfano Google Nexus 7 inayotumia Android, pia Blackberry Playbook na nyingine nyingi, kwa mwenye bajeti nzito basi Samsung Galaxy Tab, na iPad zinaweza kuwa mfano mzuri wa kuanzia.
Tablet Kutoka Google Ni Moja ya Tablet Nzuri ya Bei Raisi. Kuanzia takribani 330,000/= |
Kwa wanaopenda utumiaji wa kadi za data (memory cards) iPad halitakuwa chagua zuri kwao, kwani hazina uwezo huo.
Kitu cha kuweka akilini ni kuwa tablet zinaitaji utunzaji wa hali ya juu, kwani kumbuka ikianguka ni kwa asilimia kubwa zinaweza pata itilafu za vioo. Nasema hivi kwa sababu mimi pia nishaathirika na janga hili.
Laptops zinapatikana katika maduka mengi katika miji yetu, sina uhakika na upatikanaji wa tablets nje ya jiji la Dar es Salaam, ila najua zinapatikana kwenye baadhi lakini nadhani bado suala la uchaguzi kwenye baadhi ya mikoa litakuwa dogo sana. Hivyo kwa mtu anayeitaji tablets ni vizuri aingie kwenye sehemu ambayo ataweza ona za aina mbalimbali ili kukusaidia katika uchaguzi bora ziadi kulingana na bajeti na mapendeleo yako. Na hili linawezekana kwa Dar es Salaam.
Rudi Tena Kwa Toleo Namba Mbili la Turudi Shule tutaangalia sekta ya simu na modem za intaneti, na hii ni pamoja na kuangalia je ni mtandao gani wa simu uchague kwa huduma za intaneti kulingana na matumizi yako.
Tunawatakia likizo nzuri na maandalizi bomba ya mwaka wa masomo unaotangulia, kumbuka kusambaza makala hii kwa wengine! Pamoja!
NB: TUNATEGEMEA KUONGEZA VITU KWENYE HII MAKALA..
No Comment! Be the first one.