CEO – Mkurugenzi mkuu wa kampuni mashuhuri ya vifaa vya elekroniki ya Apple, Bwana Tim Cook amejitangaza kuwa ni shoga!
Bwana Cook amejitangaza rasmi kupitia makala aliyoandika katika mtandao wa BusinessWeek wiki hii, masaa machache tu yaliyopita. Watu wengi washawahi kuelezea wasi wasi wao kuwa CEO huyo anaweza kuwa ni shoga lakini hii ni mara ya kwanza yeye mwenyewe kulielezea jambo hilo.
Katika makala hiyo Bwana Cook amesema kama ‘kusikia ya kwamba CEO wa kampuni kubwa kama Apple ni shoga kutawasaidia wengine waliokwenye hali hiyo kujikubali na kutosita kujitokeza basi ameona inathamani ya yeye kujitangaza’.
Inasemekana wafanyakazi wengi wa kampuni hiyo ya Apple tayari walikuwa wanafahamu ya kuwa Bwana Cook ni shoga, hakuwaficha na amesema anafurahi kwani utamaduni wa Apple ni mzuri na usio tenga watu kutokana na tofauti zao.

Je suala hili litaathiri mtazamo wako kwake na kwa kampuni hiyo?
No Comment! Be the first one.