Simu janja za Tecno zipo lukuki sokoni na zina wateja wengi sababu rahisi ni kwamba bei yake inahimilika (rahisi). Unakumbuka Tecno Phantom? Sasa ni toleo la kenda (9).
Wateja wengi wa simu janja wanaweza kuwa kwenye wakati mgumu hasa akiwa ni mpenzi wa rununu za Tecno kutokana na kwamba zipo nyingi sokoni vilevile sifa zake zinavutia. Sisi kama wafuatiliaji wa masuala ya teknolojia tukakutana na habari kwamba toleo la kenda kutoka familia ya Phantom limetoka.
Dhima kuu ya kauli hii ni kuwa hakikishia watumiaji wasimu za TECNO juu ya ubora na uimara zaidi utakaoletwa na kumpuni hii pendwa nchini na kwenye bara kwa ujumla. Kwa sasa, TECNO inashika nafasi ya 5 Afrika kama kampuni ya simu pendwa.
Sifa kamili za Phantom 9 ni kama ifuatavyo:-
NETIWEKI | Teknolojia | GSM / HSPA / LTE |
---|
UZINDUZI | Tangazo | Julai,2019 |
---|---|---|
Rasmi | 25 Julai 2019 (Kwa Tanzania) |
JUMBA | Ukubwa | 158.5 x 75.3 x 7.9 mm (6.24 x 2.96 x 0.31 in) |
---|---|---|
Uzito | 164.4 g (5.78 oz) | |
Laini | Laini Mbili (Nano-SIM) |
KIOO | Mfumo | AMOLED capacitive touchscreen, 16M colors |
---|---|---|
Saizi | 6.39 inches, 100.2 cm2 (~84.0% screen-to-body ratio) | |
Ubora | 1080 x 2340 pixels, 19.5:9 ratio (~403 ppi density) | |
Ulinzi Wa Kioo | Corning Gorilla Glass 3 |
UENDESHAJI | OS | Android 9.0 (Pie) |
---|---|---|
Chipset | Mediatek MT6765 Helio P35 (12nm) | |
CPU | Octa-core (4×2.3 GHz Cortex-A53 & 4×1.8 GHz Cortex-A53) | |
GPU | PowerVR GE8320 |
UJAZO | Memori Kadi | microSD, mpaka TB 1 (unaweza ukaongeza mwenyewe) |
---|---|---|
Ujazo Wa Ndani | 128 GB, 6 GB RAM |
KAMERA KUU | Kamera Tatu | 16 MP, f/1.8, PDAF 8 MP, f/2.4, 13mm (ultrawide) 2 MP, f/2.8, depth sensor |
---|---|---|
Sifa Zake | LED flash, HDR, panorama | |
Video | 1080p@30fps |
KAMERA YA MBELE | Moja | 32 MP, f/2.0 |
---|---|---|
Sifa Yake | HDR | |
Video | 1080p@30fps |
SAUTI | Loudspeaker | Ndio (Ipo) |
---|---|---|
3.5mm jack | Ndio (Ipo) |
TEKNOLOJIA MAWASILIANO | WLAN | Wi-Fi 802.11 a/b/g/n/ac, dual-band, Wi-Fi Direct, hotspot |
---|---|---|
Bluetooth | 5.0, A2DP, LE | |
GPS | Ndio, inakuja na A-GPS | |
Radio | FM radio | |
USB | microUSB 2.0, USB On-The-Go |
VIPENGELE VINGINE | Sensa | Fingerprint (tena kwenye kioo), accelerometer, gyro, proximity, compass |
---|
BETRI | Betri halitoki | Li-Ion 3500 mAh |
---|
Nisikuchoshe sana, hakika simu hii imekuja na muundo wa kipekee na mzuri zaidi wa kuvutia. Kilicho nivutia mimi zaidi ni Kamera tatu za nyuma, kamera ya mbele, kioo kikubwa na kizuri zaidi chenye muundo wa “dot notch” kwa juu pale katikati.
Tumekua tukiona makampu ni mengi ya simu yakiondoa tundu la kuchomeka earphone; lakini hapa kwenye Phantom 9 TECNO wameona watuachie “earphone jack” ambayo ipo upandewa chini wa simu hiyo.
We unaona ni jambo gani limekuvutia sana kutoka toleo hili?Endelea kutufuatilia kwa ajili ya kupata sifa nyingine nyingi pamoja na maelezo ya undani kabisa kuhusiana na TECNO Phantom 9.
Ningependa Kusikia Kutoka Kwako, Niandikie Hapo Chini Katika Sehemu Ya Maoni Wewe Umevutiwa Na Kipi, Pia Kumbuka Kutembelea TekoKona Kila Siku Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!