Ni wazi kuwa makampuni mengi hivi sasa yanapambana sana katika kuhakikisha wanapata faida huku kazi zao zinaenda kama kawaida katika kipindi hichi kigumu, Moja kati ya kampuni hizo ni Spotify.
Vile vile ni wazi kuwa dunia nzima katika upande wa biashara au uchumi kwa ujumla inapitia pagumu kwani kwa sasa kuna kushuka kwa uchumi
Mpaka sasa kampuni ya Spotify haijasema dhahiri kuwa ni vitengo gani kabisa ambavyo vitaathiriwa moja kwa moja na maamuzi hayo
Kwa makampuni kama vile Twitter, na Meta inayomiliki Facebook walitangaza kupunguza nafasi za ajira katika makampuni yao miezi ya nyuma tuu.
Ukiachana na hayo kuna makampuni mengine mengi tuu ya kitekonolojia ambayo yalifika mbali Zaidi na kuweza kusitisha (kuwapunguza) watu ajira mfano kampuni ya Netflix.
Kwa kipindi cha miaka ya nyuma wafanyakazi walikua wakiongezeka kwa miaka hadi miaka kwa asilimia kubwa lakini kwa mwaka 2022 hali imekua gumzo.
Spotify bado ni miongoni katika kampuni maarufu na kubwa inayojihusisha na maswala ya usambazaji wa muziki na burudani zingine.
Niandikie hapo chini katika uwanja wa comment, kwa hali jinsi unavyoiona na makampuni mengi bado yanazidi kupunguza wafanya kazi na nafasi za kazi unadhani itatulia hivi karibuni au tutaona mengi?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.