TECNO nao bado hawalali, imetangaza kuja na App ya huduma za kifedha ambayo inaitwa TECNO Wallet.
App hii kwa mara ya kwanza kabisa itaanza kufanya kazi katika toleo jipya la Tecno Camon 19 ambalolitatoka hivi karibuni.
Kazi kubwa ya app hii ni kusaidia watumiaji wa simu za TECNO kuweza kufanya miamala, kulipia bili na mambo mengine mengi tuu
Ndani Ya App Kuna Vitu Kama;
- Mfumo mzima wa malipo wa kidijitali
- Unaweza nunua muda wa maongezi, intaneti na kufanya manunuzi mengine mbalimbali ya kila siku
- Vile vile unauwezo wa kupata huduma nyingine nyingi za kifedha kupitia app hiyo
- Unaweza kupata mikopo kwa haraka Zaidi
- Kama ikitokea kuna promosheni kama na wewe ni mtumiaji wa App hii kuna hati hati kubwa kuwa na wewe utahusishwa.
Kwa matoleo mengine ya simu inabidi washushe App hii kupitia soko la Google Playstore, lakini kwa watakao kuwa wanatumia toleo la Comon 19 basi watakuta App hii iko ndani ya simu hizo tayari.
Kwa sasa tuishie hapo lakini tutaendelea kukujuza Zaidi pindi tukipata habari Zaidi juu ya App hii.
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini kwenye uwanja wa comment, hii umeipokeaje? Je unadhani huduma hii kwa Tanzania itafanikiwa.
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.