Paka ni moja ya viumbe maarufu sana katika mitandao ya kijamii baada ya binadamu. Na uhakika ushakutana na picha na video kadhaa za paka katika pitapita zako. Kiongozi mmoja wa kidini nchini Saudi apiga marufuku watu kupiga picha za selfi na viumbe hao.
Kiongozi huyo (Cleric) bwana Saleh bin Fawzan al-Fawzan ni mmoja wa wajumbe wa baraza la kidini lenye nguvu sana nchini humo – Saudi Council of Senior Scholars.
Picha/video za paka, na picha za selfi na paka ni maarufu sana mtandaoni.
Picha ya utani
Bwana Fawzan amesema ‘kupiga picha na paka ni tabia inayosambaa sana kwenye watu wanaopenda kuwa kama wazungu’ (alitumia neno ‘westerners’, yaani watu wa mataifa ya magharibi – Ulaya na Marekani.
Kiongozi huyo aliliongelea jambo hilo baada ya kuulizwa swali kuhusu mtazamo wako juu ya jambo la upigaji picha za selfi alipokuwa anahojiwa katika kipindi cha televisheni.
Baadaye alipanua zaidi tafsiri yake akisema upigaji picha wa aina yeyote kama hauna maana si wa lazima. Alisema isiishiye kwenye paka tuu bali ata na mbwa au kingine chochote kisicho cha ulazima/maana.
Mbunifu na mpenda teknolojia.
Muanzilishi wa Teknokona, TechMsaada na Teknokona Group LTD - WWW.TEKNOKONAGROUP.COM
Muda wangu umegawanyika kati ya kazi kibunifu @teknokonagroup na uandishi wa habari za Teknolojia hapa Teknokona Blog.
| mhariri(at)teknokona.co.tz |