Mwaka 2018 kampuni ya Microsoft ilikua haifanyi vizuri, hali ambayo iliathiri kwa kiasi kikubwa wanunuzi katika kampuni hiyo.
Timu hiyo ya watu wasiopungua 200 iliundwa rasmina Microsoft katika hatua za kuhakikisha kuwa wanunuzi wanarudi kwa tena kwa kiasi kikubwa katika kampuni hiyo.
Timu hii ilivyoundwa iliundwa na ilikua na wafanya kazi wa kawaida kabisa (wenye maisha ya kawaida) na wenye uzoefu wa kawaida kabisa.
Hii sio mara ya kwanza kwa Microsoft kupunguza baadhi ya watu wanaofanya kazi katika kampuni hiyo na hata uajiri wake wa wafanya kazi wapya umeshuka sana.
Kwa hao 200 ambao wamepunguzwa hapa kampuni inawashauri waombe maombi katika kampuni (hii ni kama kuna nafasi wanazofuzu) au kama imeshindikana waanze kutafuta sehemu nyingine.
Vifaa au huduma ambazo ziliwafanya Microsoft kuunda timu maalumu ya kuleta wateja ni Windows, Microsoft 365, Microsoft Teams for consumer, Surface, na Xbox
Lakini kingine kama unakumbuka vizuri timu hii iliundwa mwaka 2018 na hii ni baada ya kampuni hiyo ilikua imetoka/ina pitia katika kipindi kigumu sana
Kumbuka mwaka 2017 kampuni iliachana kabisa na biashara yake ya kutengeneza na kuuza simu (simu za Microsoft Lumia), mwaka huo huo wakaachana na huduma yao ya Kinect na baadhi ya bidhaa nyingi tuu kuwa zimekufa au wameachana nazo.
Lakini kwa sasa bado kampuni inafanya mambo mengi sana katika kuhakikisha kuwa inarudi katika hali nzuri na kuanza kupata mapato yanayoridhisha kama zamani
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika eneo la comment, je hili umelipokeaje? Ni sawa kuipunguza timu hiyo?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.