Tangia uwezo wa ‘3D Touch’ kutambulishwa katika simu za iPhone 6s na zile zingine za mbele ilikua ni teknolojia ngeni katika soko la simu janja. Hivi sasa Apple wana mpango wa kuachana na teknolojia hiyo na kuja na mpya.
Uwezo wa ‘3D Touch’ utauliwa katiak simu zote za iPhone ambazo zitatoka katika mwaka 2019 na kuendelea. Teknolojia hiyo itapata mbadala wake anaejulikana kama ‘Haptic Touch’
‘Haptic Touch’ kwa mara ya kwanza ilitambulishwa katika toleo la (kwanza) mwaka jana la iPhone XR. Ikumbukwe kwamba hapo nyuma teknolojia ya ‘3D Touch’ ilianzishwa huku ikiwa inafanya kazi kwa kuhisi aina ya mguso katika skrini ya simu ili kutoa chaguzi mbali mbali kama ikiwa ni njia ya mkato kabisa. Mtu ulikuwa unaweza chagua cha kufanya katika App yeyote kabla hata hujaingia katika App hiyo.
‘Haptic Touch’ yenyewe haingalii ni kwa nguvu kiasi gani umegusa skrini kama ilivyo ‘3D Touch’ bali yenyewe inaangalia ni kwa muda gani umegusa kioo katika sehemu (husika unayotaka).