Unaweza ukadhani ni masihara lakini ni kweli na imewezekana; mkojo waguzwa na kuwa pombe kwa kutumia mashine inayotumia umeme wa Jua.
Watafiti kutoka chuo cha Ghent wametengeneza mashine yenye uwezo wa kutenganisha mkojo katika sehemu mbili; maji na mbolea. Watafiti hao walikusanya lita 1,000 za maji ndani ya siku 10 na wanatarajia kutumia maji kutengeneza pombe.
Mashine hiyo yenye kutumia umeme wa Jua ina uwezo wa kutoa maji ya kunywa na mbolea kutokana na mkojo. Mabaki yanapatikana baada ya mchakato mzima kukamilika inaweza kutumika kama mbolea.
Jinsi inavyotengenezwa
Mkojo huo unachujwa kwenye mashine hiyo na kisha kisha kujitenga na mabaki yake; Nitrojeni na Phosphorus kutumika kama mbolea. Watafiti hao wanategemea kutumia maji kutengeneza bia.
Katika utafiti huo umeonekana mkojo unaweza kutumika kwa matumizi mengine ambapo soksi inaweza kutumika kutuma sms wakati wa dharula kwenda kwenye mashine pale ambapo mashine hiyo inatumia mkojo kama chanzo cha nguvu ya umeme kwa kutumia kifaa walichokiita ‘Pee power‘.
Lengo ni kutumia chanzo kisafi cha umeme kama vile kutumia umeme utokanao na haja kubwa chooni kwa vijijini ambavyo teknolojia hiyo itasaidia katika utunzaji wa mazingira kwa kiasi kikubwa na vituo vya kuchaji kwenye kambi za wakimbizi.
Je unalionaje jambo hili?
Vyanzo: Telegraph.co.uk, mitandao mbalimbali.
One Comment
Comments are closed.