Google Pixel 4a ni moja ya simu janja ambayo imezika kwa kiasi kikubwa na hivyo kuinua kimapato kampuni iliyozitengenza. Google wameamua kuiondoa kabisa simu hiyo kwenye duka lake. Je, unajua ni kwanini?
Kwa muda mrefu simu janja-Google Pixel 4a imekosekana dukani kutokana na kuuzika mpaka kuisha kutokana na kupatikana kwenye masoko mbalimbali duniani lakini sasa Google wameona waiondoe kabisa dukani kwao. Simu hii ilizinduliwa mwezi Agosti 2020 baada ya mpngo wa awali kupigwa kalenda kwani ilikuwa ikitazamiwa kutoka kati ya mwezi Aprili au Mei ya mwaka huo lakini mambo yakawa tofauti.
Baada ya simu hiyo Google wakaanza kutoa mwendelezo simu janja (Pixel 4a 5G, 5) kwa kulenga masoko fulani fulani hasa Marekani na Japan. Hii inatokana na uhaba wa upatikanaji wa vifaa ambavyo vimeifanya Google kushindwa kutengeneza rununu nyingi zaidi na kuziuza kwenye masoko mengine duniani.
Hivi sasa Pixel 5a 5G ndio simu ya bei rahisi zaidi kwa sasa kutoka Google ikipatikana kwa $449|zaidi ya Tsh. 1,032,700 bei ya ughaibuni. Baadae mwaka huu Google wanatazamiwa kutoa Pixel 6a ambayo kwa habari za chini chini sifa zake zimeshavuja.
Je, wewe ni mmoja kati ya watu ambao wanatumia simu hii ya Google ambayo kwa sasa inapatikana kwa nadra sana? Tuambie na kumbuka kutufuatilia kila inapoitwa leo.
Vyanzo: GSMArena, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.