Siku ya jumatano Instagram imeachia toleo jepesi (Lite) ambalo limeanza kupatikana kwa watumiaji wa Android.
Instagram imeamua kuachia toleo hilo jepesi ikiwa ni maalumu kwa nchi zinazoendelea na watu wengine duniani ambao wanatumia simu ambazo zina nafasi ndogo pamoja na maeneo ambayo kuna matatizo ya mtandao.
Ukiwa na toleo jepesi (Lite) la Instagram utaweza kufanya mambo yote kama mtumiaji wa kawaida mwenye programu tumishi halisi.
Mambo ambayo hautaweza kufanya kwa sasa ni kupakia video pamoja na kusambaza ujumbe (message) kwa njia ya kushirikisha moja kwa moja kwa marafiki jambo ambalo uongozi wa Instagram umeeleza upo kulifanyia kazi zaidi.
Instagram Lite inategemea kuongeza zaidi watumiaji wa Instagram hasa kutoka nchi zinazoendelea kama Tanzania.
Instagram Lite itawawezesha watumiaji kuweza kufurahia namna rahisi zaidi ya kupakia picha huku nafasi katika simu zao ikiwa ya kutosha na hivyo kuleta urahisi zaidi wakati wa utumiaji.
Kutokana na toleo hilo, kuna uwezekano mkubwa wa ongezeko la watumiaji hasa kutoka nchi zinazoendelea ambazo zimekua zikikumbwa na matatizo ya kimitandao pia na uwepo wa vifaa duni ambapo kwa toleo hili itakua rafiki kwao.
Kwa sasa imeanza kupatikana nchini Mexico, lakini siku zijazo itaanza kupatikana duniani kote.
Timu ya uandishi wa Kona ya Teknolojia ingefurahi kupata sapoti yako ili iendelee kukuletea habari na maujanja mbalimbali.
Wezesha bando kwa kutuma kiasi chochote kupitia Selcom, kwenye simu yako bofya *150*50*1# kwenye namba ya malipo weka 60751369 jina litakuja TEKNOKONA.
One Comment
Comments are closed.