Ijue simu janja ya kwanza kutengenezwa ambayo inaweza kuoshwa na sabuni, simu hiyo iliyotengenezwa na kampuni ya kijapani ya KDDI simu hiyo inayo kwenda kwa jina la “Digno rafre” inategemewa kuzinduliwa siku chache zijazo.
Ndio zipo simu janja nyingi ambazo zinauwezo wa kuzuia maji kuingia ndani ya simu lakini hii itakuwa ni simu ya kwanza ambayo itaweza kusio tu kuzuia maji kuingia ndani bali hata kama utataka kuiosha na sabuni basi utaweza kufanya hivyo bila kuwa na wasi wasi na kuiharibu.
Simu hiyo inayotegemewa kuuzwa kwa karibu dola 175 za kimarekani (Takribani laki nne za sh) na pengine itauzwa Japani tu kwa sasa. Watengenezaji wa simu hii wanawalenga hasa wazazi ambao wanawatoto wadogo ambao ni rahisi kuchafua simu zao.
Simu hiii hata hivyo itaweza kuhimili kuoshwa na baadhi ya sabuni sio kila sabuni, katika tangazo ambalo watengenezaji wa simu hiyo wameliweka mtandaoni mtoto anadondosha simu katika chakula na mama yake anaonekana akiiosha katika bomba na sabuni kisha baadaye mtoto anaonekana akichezea simu bafuni.
Teknoloji inayotumika hapa ni ile ya kuzuia maji kuingia ndani ya simu lakini imeongezwa pia uwezo wa kuzuia povu na sabuni, screen yake kwa upande mwingine ni kwamba inaweza kutumiwa hata na mikono mibichi.
One Comment