Facebook imenunua kampuni maarufu ya kutengeneza picha zinazojongea maarufu kama GIF. Kampuni hiyo inakwenda kwa jina la Giphy.
Ni wazi kuwa Giphy ni kampuni ambayo imejikita tuu katika picha mjongea, FB imenunua kampuni hiyo lakini taarifa nzima za dili hilo halikuwekwa wazi, japokuwa kuna vianzo vingine vimesema kuwa ni takribani dola mia 4 za kimarekani.
Kumbuka Giphy ni kama mtandao wa kijamii tuu ambao unatumika ku’share’ picha jongefu kwa ndugu, jamaaa na marafiki.
Kwa mujibu wa Facebook, lengo la kuinunua kampuni hiyo ni kuiunganisha na kampuni yao ya Insatgram. Kwa mantiki hiyo ni kwamba tarajia kuona GIF kama kipengele ndani ya mtandao wa Instagram ndani ya siku zijazo.
Ukiachana na hayo FB wameweka wazi kuwa kampuni ya Giphy itakuwa inajitegemea kwa kufanya kazi nje ya vipengele vya Facebook. Vile FB imewaka wazi kuwa watu wengi wanautumia Giphy huwa watoka katika mtandao ya kijamii ya Instagram, Facebook, Messenger na WhatsApp na mara nyingi huwa wana’share’ GIF hizo katika mitandao hiyo.
Niambie wewe unahisi baada ya kampuni hii kununuliwa Facebook itabadilika katika nyanja gani? niandikie hapo chini katika eneo la maoni. Pia kumbuka kutembelea TeknoKona kila siku kwani daima tupo na wewe katika teknolojia!.