Hivi unajua huduma ya Apple TV+ ya ku’steam’ ilikua inaruhusu mtu kufanya majaribio huduma hiyo kwa kipindi cha mwaka mzima kisha ndio kuamua kuanza kulipia.
Ni wazi kuwa kwa mwaka mzima bado ni kipindi kikubwa sana na kinaweza kufanya kampuni kukosa mapato mengi tuu. Apple wameamka maana hili linabadilika mwezi ujao.
Kuanzia tarehe moja ya mwezi wa 7 2021 huduma hii itakuwa na kipindi cha majaribio cha miezi mitatu tuu tofauti na mwanzo.
Ni wazi kuwa Apple TV+ inazidi kujiimarisha zaidi kwani wanazidi kuongeza programu ambazo zinafanya vizuri na zina majina makubwa.
Hii ni ikiwa moja ya njia ya kuwavutia watu wengi zaidi kuingia na kujiunga katika huduma hiyo.
Lakini huduma hii haipatikani tuu (na ilikua haipatikani tuu) ili kupatikana kwa huduma hii ilikua ni lazima uwe unatumia kifaa kipya kabisa na kisha uunganishe na akaunti ya Apple (Apple ID).
Hii inajumuisha vifaa vyote ambavyo ni vipya kabisa vya iPhone, iPad, iPod touch, Apple TV or Mac. Huduma hii kama kawaida isipokua inapatikana huku (kwetu) lazima ianze kwa wenzetu huku sisi tukisubiri.
Chanzo: Chapisho Kutoka Apple!
No Comment! Be the first one.