Miaka ya zamani sana asa kwenye nchi za ulaya na nyingine watu walikuwa wanaandika ujumbe kisha kuuweka ndani ya chupa na kuifunga kisha kuitupa baharini wakiamini kuna siku ujumbe huo utasomwa… Ni kutokana na hilo ndio likafanya watu waje na app inayoitwa Fling.
App hii inakuwezesha kutuma picha, video na ujumbe wa sms kwa hadi watu 50 mahali popote duniani. Pale unapoandika na kutuma ujumbe huo utakuwa ata hufahamu utawafikia wakina nani na katika nchi gani, wapokeaji wakipenda ulichowatumia basi nao wanaweza kukujibu na mkazidi kuwasiliana.

Kama ulikuwa unasiri unatamani kumwambia mtu basi nafasi ndio hii 😉 …pia kama wewe ni mtu unayependa kutengeneza marafiki wapya duniani kote basi pia app hii inaweza ikawa inakufaa.
Bofya kuipakua Kwenye Simu/tableti – Android | iOS
No Comment! Be the first one.