Kampuni ya mauzo ya mitandaoni, Amazon inapanga kuunda programu ya kujipima mavazi kabla ya kununua japo si moja kwa moja itakayotumika kwenye simu janja.
Programu hiyo itahitaji kuwa na ufahamu wa mambo ya kimsingi ya mtu na itakagua picha za mteja kupitia mitandao ya kijamii kisha kupendekeza mavazi ambayo yanaweza kumfaa zaidi.
Baada ya ukaguzi huo, kampuni hiyo itapendekeza nguo ambazo mteja anaweza kufurahia. Aidha, itapendekeza mavazi ya mtu kulingana na eneo analoishi na kazi anayofanya.
Kwa kupitia picha za mteja, kampuni inaweza kuona wanachovaa, wanachoendesha na hata ndani ya nyumba zao ili kubashiri kitu ambacho mteja anawezakupenda sana kukinunua. Programu hiyo itakagua picha ili kubaini sehemu za mwili ambazo zitaunda taswira nzuri.