Simu tunazonunua zina vitu vingi ambavyo si rahisi kuvifahamu kwa mara moja au tusifahamu kabisa tusipokuwa watu wa kupenda kujua mambo mengi kwenye vifaa tunavyomiliki na moja kati ya vitu hivyo ni maana ya “TTY Mode” kwenye rununu.
Teknolojia inakua kila uchwao ikitoa tafsiri kwamba watu wanabuni namna ambavyo kitu watakachokileta kitasaidia makundi yote ya watu na kadri siku zinavyosogea ile dhana ya kwamba kundi fulani limesahaulika inapotea, nitakwambia kwanini.
“TTY Mode” au “Tele Type Writer/Text Telephone” ni mfumo wa simu ambao unasaidia watu wenye ulemavu wa kusikia au matatizo ya kuongea kuweza kuelewa kitu kilicho katika mfumo wa sauti.
Sasa kwenye simu janja mbalimbali (LG, Samsung, n.k) unaweza kuwa umeshakutana na kipengele hicho ukawa unajiuliza “Kina kazi gani?”. Kwa kuwa umeshafahamu kuwa kinasaidia/ni mahususi kwa wale ambao wana matatizo ya kusikia/kuongea ni vyema ukatambua kuwa iwapo ukiruhusu kipengele hicho basi huduma kama ujumbe mfupi wa maneno, kuelewana na mtu akikupigia vinaweza visifanye kazi vyema.
Hivyo ndivyo teknolojia inavyosaidia hata makundi yenye mahitaji maalum ingawa inawezekana kabisa ni kundi dogo tu la walengwa ndio wanaofahamu kuhusu jambo hilo. Usisite kushirikisha na wengine.
Vyanzo: Tech Junkie, Tech Walla
One Comment
Comments are closed.