Pengine soko la simu janja za kujikunja lilikua halitegemewi kukua kwa kasi kama inavyoonekana, makampuni mengi yanahakikisha kuwa yanaweza simu zenye teknolojia hii sokoni na sasa ni zamu ya Vivo.
Vivo ni moja kati ya kampuni za kuuza na kutengeneza simu janja inayofanya vizuri sana kwa mwaka 2022 imeshika nafasi za juu kabisa katika makampuni ambayo yameongoza katika mauzo ya simu zake.
Kwa sasa kuna makampuni mengi ya simu yanaingia katika soko la namna hii, Samsung wenyewe ambao ndio wanaongoza katika soko hili wanadai kuwa wanataka kuzifanya simu zao za kujikunja kuuzika zaidi angalau hata kufikia nusu ya mauzo ya simu janja zao za kawaida.
Turudi kwa Vivo, pengine hii inaweza ikawa ndio mshindani mkubwa wa simu za kujikunja kutoka Samsung (Galaxy Fold).
Simu ambayo kampuni itaitambulisha vyanzo mbalimbali vinasema kuwa inajulikana kama Vivo X Fold S, na simu hiyo itakua na vipengele vya ziada ikilinganisha na Vivo X Fold ambayo tayari ipo sokoni.
Sifa zinazotegemewa kuwepo katika simu hii mpya ni chipu ya Qualcomm (Snapdragon 8+ Gen1), betri la uwezo wa mAh 4,700. Chaja ya haraka (fast charging) inayopitisha 66w.
Vile vile vyanzo mbalimbali vinadai kuwa watu wasitegemee simu hii kuwa na mambo ambayo yatawashangaza sana ukilinganisha na ile ya kwanza.
Lakini kingine ni kwamba hata ukifuatilia majina yake tuu unabaini kwamba hakutakua na mambo mengi mapya katika simu hii, hali kama hii tumeishaizoea sana kwa makampuni kama Apple Samsung n.k
Ningependa kusikia kutoka kwako, naindikie hapo chini katika eneo la comment, je unadhani ni sawa kwa Vivo kuja na simu janja ya kujikunja huku ikiwa haina vipengele vipya vya kushangaza ukilinganisha na ile ya mwanzo?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.