Moja kati ya makampuni makongwe kabisa katika kuzalisha na kuuza simu ni sony, simu zake ziliingia sokoni na kupata jina kubwa sana, ukiachana na hayo bado kampuni inajihusisha na mambo mengi katika teknolojia.
Kwa sasa kampuni ya Sony imetoa tangazo ambalo linasema kuwa mwezi septemba mwaka huu kutakua na uzinduzi wa simu.
Vyanzo mbalimbali vinadai kuwa simu hiyo itakua ni Sony Xperia 5 IV, lakini kingine cha kushangaza ni kwamba kampuni hii ya japani haijaweka mambo wazi juu ya kifaa inachoenda kukizindua.
Kupitia mtadao wa Twitter kampuni iliweza kutoa tangazo hilo na kusema kuwa kuna habari kubwa inakuja.
Big news is coming!
Subscribe to @SonyXperia YouTube to watch our exciting announcement on September 1st 2022, 16:00 Japan Time / 9:00 CEST. #Sony #Xperia #SonyXperia #ProductAnnouncement
— Sony | Xperia (@sonyxperia) August 25, 2022
kwa sasa hukuna taarifa zozote kuhusiana na kifaa hiki ila kutokana na toleo la nyuma ni kwamba simu hiyo inaweza ikaja na chipu ya Qualcomm, refresh rate ikawa ni 120Hz, kioo cha FHD+OLED
pengine kamera yake ya mbele inaweza ikawa ni 12MP, huku za nyuma zikiwa ni 12MP ikiwa na uwezo wa kuchukua eneo kubwa na 12MP yenye uwezo wa kuvuta (ku’zoom) kwa mbali zaidi.
Hapa cha muhimu zaidi ni kusubiri mpaka kifaa hiki kikitambulishwa sokoni mwezi septemba maana ndipo ambapo tutajua sifa zake kwa undani kabisa na hata muonekano wake.
Pengine ulikua unaona kama kampuni imelala sio? Hili linakuja kubadilika kwani kampuni bado ipo katika mchakamchaka wa kuhakikisha kuwa inazidi kuwapa wateja wake kile wanachohitaji.
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika eneo la comment, je ushawahi kutumia simu za Sony Xperia? Vipi uozefu wako na vifaa hivi?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.