Hivi namba za simu zinaweza kuisha kweli? Japan kuishiwa namba za simu za kuweza kutumika na hivyo wamekuja na mfumo mpya wa kuweza kutengeneza namba za simu nyingine zaidi.
Namba mpya zinazokuja zitakuwa ndefu zaidi (tarakimu 14) kuliko zile za nyuma (tarakimu 11). Namba hizo mpya zinatarajiwa kuwa tayari na kuanza kutumika pindi ifikapo mwanzoni mwa 2021 hiyo ni kwa sababu namba ambazo zinatumika sasa zinatarajiwa kuisha ifikapo 2122.
Mitandao mikubwa ya nchi hiyo imeshakubaliana na hili wazo la kutengeneza namba zingine za simu. Mitandao kama NTT Docomo, KDDI, na SoftBank imejadiliana kuwa kwa kuanzia waje na namba bilioni 10 (za tarakimu 14).

Teknolojia ya 5G inategemea kuanza kutumika rasmi Japan ifikapo mwaka 2020 hivyo ni wazi kwamba utumiaji wa laini katika vifaa vya intanet utaongezeka kwa kiasi kikubwa sana na ukifutatilia vizuri jambo hili ndio linalofanya kwa kiasi kikubwa kuwe kuna uhitaji mkubwa wa namba zingine.
Makubaliano ya kuja na mfumo mpya wa namba za simu za Japan ili kuwezesha laini bilioni moja zingine umehusisha mazungumzo ya vyombo vya serikali na wadau wengine wote muhimu – hii ikiwa ni pamoja na mitandao ya huduma za simu.
Lakini tatizo hili sio la kwanza kuikumba Japan tuu hata UK kuna kipindi waliongea namba kwa baadhi ya maeneo baada ya wa watumiaji wa maeneo hayo kuishiwa na namba za simu.