Licha ya kampuni ya Huawei kushutumiwa na vita ya kiusalama ambayo imesababisha kampuni hiyo kuwakosa Google na makampuni mengine kama vile Qualcomm, bado imeinua kifua mbele na kusema jambo hilo bado halitawarudisha nyuma kama watu wengi wanvyodhani.
Bwana, Ren Zhengfei amabe ndio mwanzilishi wa Huawei amesema kuwa kampuni yake licha ya kupata changamoto kama hizo (kuwakosa Google) bado itajikita zaidi katika kujiendeleza na kuzidi kuwa juu kwa sababu wana mikakati mingi sana ili kufanikisha hilo.
“Katika kipindi hichi kigumu napenda kushukuru makampuni kama vile Google na mengine kadha wa kadha ambayo kwa namna moja yameisaidia Huawei kukua na kujiendeleza” – Ren, aliongezea.
Mkuu wa Huawei pia alishawahi sema kuiunga mkono na kuisapoti kampuni sio lazima mtu anunue simu toka katiaka kampuni hiyo. Hata yeye ana jamaa ambao wanatumia simu zingine lakini wanamuunga mkono yeye na kampuni yake.
Supporting #Huawei does not necessarily mean you should buy a #Huawei smartphone. My family members use #Apple for a very long long time: Ren Zhengfei, founder of China’s Huawei Technologies (Photo: Chen Qingqing/GT) pic.twitter.com/5rcrHJx3KR
— Global Times (@globaltimesnews) May 21, 2019
Mkuu wa Huawei huwa sio mtu ambae anapendelea kuonekana na jicho la jamii akiwa anafanya mahijiano lakini safari hii anakiri kulikua hakuna jinsi kwani mambo mengi yalikuwa yantokea katika kipindi cha muda mfupi.
Kumbuka Huawei bado ipo katika namba mbili kama mtengenezaji na muuzaji wa simu janja, baada ya kushika namba mbili ndio kashfa hii ikaja, baada ya hiyo Google nao wakaamua hivi lakini bado kampuni imeweka kifua mbele kuonyesha kwamba hivi ni vitu vya kawaida sana katika biashara.
Ifahamike kwamba Huawei hawategemei tuu katika biashara ya kutengeneza na kuuza simu, bado wana biashara zingine kama vile kuuza teknolojia, bidhaa nyinginezo za kidijiti.