Hapa tunawaongelea watoto ambao wako chini ya umri wa miaka 16, mtandao wa instagram unatambua watoto hao kama chini ya umri na kwa sasa maudhui yao yanatolewa jicho la tatu.
Instagram inaamini kwamba kuna maudhui ambayo hayatakiwi kabisa kuonekana kwa vijana wenye umri wa chini ya miaka 16—ambao ni jambo jema kabisa.
Ni wazi kuwa maudhui yapo ya aina nyingi sana katika mitandao ya kijamii, vile vile mitandao ya kijamii ni moja katika ya vitu ambavyo vinaongoza sana katika uharibifu wa maadili kwa watoto.
Mtandao wa instagram umeliona hili na umeamua kuja na kipengele ambacho kitafanya watoto wa chini ya umri wa miaka 16 kuweza kupata maudhui ambayo wanaendana nayo kwa kiasi kikubwa.
Kizuri kutokana na jambo hili ni kwamba sio kwamba kipengele hiki kitafanya kazi katika eneo la ‘explorer’ tuu basi ni ndani ya mtandao mzima, mpaka maeneo ya search nakadhalika.
Hii sio mara ya kwanza kwa mtandao wa kijamii wa instagram kuja na mbinu mbalimbali ambazo zitahakikisha ulinzi na usalama wa mtoto unazingatiwa au unapewa kipaumbele.
Kingine kizuri ni kwamba hata kama wewe sio mtoto ila unaona kabisa maudhui unayoyapata katika mtandao huo haupendezwi nayo unaweza kubadilisha.
Ingia katika Profile, na kasha ingia katika eneo la Settings, nenda mpaka kwenye account. Ingia katika eneo la Sensitive Content Control. Ukiwa hapo ndipo unaweza kubadilisha namna ya kupokea maudhui katika mtandao huo.
Ningependa kusikia kutoka kwako, naindikie hapo chini katika eneo la comment, je wewe unaona ni sawa tuu jinsi unavyopokea maudhui katika mtandao wa instagram?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.