Kama ulisikia taarifa ya bei inayotarajiwa kuuzwa simu mpya ya iPhone X iliyotangazwa mwanzoni mwa mwezi huu bila shaka ungerudi nyuma kidogo!
Simu hiyo kutoka kampuni ya Apple inatarajiwa kuuzwa zaidi ya dola 999 za kimarekani kuanzia Novemba 3 mwaka huu, na kuifanya kuwa moja wapo ya Simu Janja ghali zaidi duniani. Takwimu za hivi karibuni zinaonyesha kuwa mwenendo wa kuendelea kupanda kwa gharama za bei ya Simu Janja umekuwa ukikua mwaka baada ya mwaka.
Kulingana na utafiti ulitolewa na kampuni utafiti kwa walaji ya kijerumani ya Gesellschaft für Konsumforschung (GfK) kwa wastani wa mauzo ya Simu Janja yanakuwa kote ulimwenguni.
Soko la Marekani linaongezeko kwa asilimia 1 kwa wastani wa upandaji wa bei tofauti na soko la Ulaya ya kati na Mashariki ambapo inaonesha kuna ongezeko kwa asilimia 26 ya upandaji wa bei ya Simu Janja. Kumbuka soko kwa Amerika ya kaskazini nalo ni kubwa, hawa wanaongezeko la asilimia 1.
Hata hivyo, takwimu zinaonesha kwamba watumiaji wa Simu Janja ghali wameongezeka kuliko ilivyokua awali kwa ulimwenguni kote. Soko la mashariki ya kati na Afrika kumekuwa na ongezeko la mahitaji ya simu kwa asilimia 8 kila mwaka sambamba na ongezeko la bei ya Simu Janja kukua kwa asilimia 5.
Takwimu hizi zimeegemea zaidi ya masoko 75 yaliyofanyiwa utafiti huo kati ya mwezi Agosti na Septemba na bei zilizoangaliwa ni zile za kuuza na sio zile za wauzaji wa mwisho. Takwimu hizo zimeonesha kwamba bei ya simu janja zinaendelea kupanda mwaka hadi mwaka.
Pamoja na kuendelea kupanda kwa bei ya Simu Janja lakini uzalishaji wa baadhi ya simu kutoka China umekuwa una nafuu kwa kiasi fulani kwa watu walio wengi. Kupanda kwa simu kumeelezwa pia ni kwa baadhi ya watumiaji kuona fahari kutumia simu za bei ya juu ili kuonesha unadhifu na kujali kilicho bora.