Je, una fahamu ya kwamba katika simu janja nyingi moja ya teknolojia ya miaka mingi sana ambayo bado inatumika ni pamoja na ile kipini spika za masikioni yaani ‘Audio jack‘?
Sehemu hiyo kwa ajili ya vifaa vya sauti ni moja ya teknolojia yenye historia ndefu sana. Teknolojia hii ilianza kujipatia uhitaji na umaarufu katika miaka ya 1870 ambapo ilikuwa inatumika katika kuunganisha laini za mawasiliano ya simu katika kipindi ambacho mfumo wa mawasiliano ya simu haukuwa wa moja kwa moja.
Yaani kama unataka kupiga simu kwenda 0754000000 basi ilikubidi upige simu Posta, halafu wao waunganishe laini yako kwenda tundu la waya utakaokuunganisha hadi kwa mtu mwenye namba hiyo. Hivyo, walihitaji mfumo wa uunganishaji waya wa kiurahisi na kiharaka na ambao hautaharibika haraka kutokana na zoezi hilo kufanyika mara kwa mara.
Kuanzia mawaka 1878, duara lake lilikuwa na ukubwa wa robo inchi (inchi 6.35mm) ila baadae ndio ukapunguzwa ukubwa na kuwa mdogo kwa ya mm 3.5 inaitwa pia “Mini jack”, “Headphone jack” au “TRS jack”, wakati ile kubwa inabeba jina lake la “Audio Jack“.
Ingawa teknolojia inakuwa lakini bado makampuni mengi wameendelea kushikilia matumizi ya kitu hicho lakini kwa makampuni kama Apple waliona mwaka 2016 ndio tamati ya kipini hicho cha spika za masikioni na kuamua kutumia teknolojia yao wenyewe.
Ukuaji wa umaarufu wa headphones za mfumo wa bluetooth unaleta ushindani dhidi ya teknolojia hii. Tayari kuna simu kadhaa zinazokuja bila eneo la audio jack. Ingawa kuna maeneo kama haya matumizi hayo yatapungua ila bado teknolojia hii inaonekana itaendelea kuwepo na kutumika katika matumizi mbalimbali ya kazi za kurekodi na kusikiliza muziki kwa miaka mingi ijayo.
Teknolojia hiyo bado inaonekana kuwa na mashiko kwa kampuni mbalimbali kuendelea kuikumbatia hadi leo. Je, unafikiri teknolojia hiyo bado inafaa?
Chanzo: BBC
No Comment! Be the first one.