Kampuni ya Trend Solar inayotoa huduma ya umeme wa kulipia usiotegemea gridi imezindua uuzaji wa vifaa vinavyotumia umeme wa Jua nchini Tanzania utakaosaidia wanaoishi vijijini kuondokana na matumizi ya mishumaa na vibatari.
Kampuni hiyo iliyoanza kutoa huduma mwaka 2017 imelenga kuwaleta watu wa vijijini katika ulimwengu wa kidijitali. Sambamba na hilo kampuni ya Trend Solar imeingia mkataba na kampuni ya Startimes inayojihusha na urushaji wa matangazo ya televisheni na redio.
Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Sarah Crooke (watatu kutoka kushoto) akiwa ameshika boksi lenye vifaa vinavyotolewa na Trend Solar kwa wateja.
Katika kuzingatia vipato vya watanzania wateja wanapewa nafasi ya kulipia kidogo kidogo hadi watakapokamilisha malipo.
Mteja atakuwa anapeleka marejesho kwa muda miezi 18; wakati anaanza atalipia Tsh. 139, 999 na kupewa huduma zote na ataendelea kulipia Tsh. 17, 999 kila wiki ndani wiki ya 78.
Mteja anaponunua mashine za umeme wa Jua, anapewa luninga ya kisasa ya inchi 24 kutoka kampuni ya Star Times, simu rununu 4G pamoja na kimemeshi (charger) ya kampuni hiyo (Startimes), tochi ya kuchaji, “Betri janja” linalotumia umeme wa Jua, taa nne aina za LED na ungo kutoka StarTimes kwa ajili ya kudaka mawimbi ya satelaiti.
Uzinduzi huo pia ulihudhuriwa na Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Sarah Crooke ambaye aliwataka wananchi kuchangamkia fursa hiyo ili kupata maendeleo na kuepukana na matumizi ya vibatari yatakayowaletea madhara kiafya.
Timu ya uandishi wa Kona ya Teknolojia ingefurahi kupata sapoti yako ili iendelee kukuletea habari na maujanja mbalimbali.
Wezesha bando kwa kutuma kiasi chochote kupitia Selcom, kwenye simu yako bofya *150*50*1# kwenye namba ya malipo weka 60751369 jina litakuja TEKNOKONA.