Mtandao wa kijamii wa Telegram unakuja na huduma ya kulipia na kujiunga na mitandao mingine katika huduma za Premium.
Huduma hii ya kulipia itaitwa Telegram Premium na ni wazi kabisa kwamba itakua na vipengele vingine ambavyo havitakuwepo kwenye Telegram ya bure.
Vipengele hivyo ambavyo vitaongezwa ni kama vile uwezo wa kuanza kupata huduma ya vipengele vipya kwanza kabla ya wengine.
Uwezo wa kuwa na stika (sticker) ambazo ni tofauti kabisa na watumiaji ambao wanatumia Telegram ambayo sio ya kulipia.
Pia ukiachana na hayo Mtandao unadai kuwa vipengele vingi vya Telegram Premium vitakua ni vya kipekee, kingine ni kama uwezo mkubwa wa kutuma mafaili makubwa kabisa
Mpaka hapo mtandao unasema kuwa hakutakua na ubaguzi mkubwa kati ya mtumiaji wa Premium kwa mfano mtumiaji wa kawaida ana uwezo wa kuweza kuona mafaili hayo makubwa kutoka kwa watumaiji wa Premium.
Vipengele ni vingi, Hivi karibuni hata mtandao wa WhatsApp na wenyewe umetangaza WhatsApp Business ya kulipia.
Kumbuka hizi ni baadhi ya njia ambazo mitandao hii ya kijamii inazitumia ili kujihakikishia kwamba ina jiongezea kipato kwa namna moja au nyingine.
Ni jambo jema kwa mtandao wa Telegram lakini ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika uwanja wa comment, je hii umeipokeaje?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.