Baada ya mafanikio kwenye Kombe la Dunia 2018 teknolojia ya Video Assistant Referee maarufu kama VAR itafanyiwa majaribio kwenye mechi za ligi kuu ya Uingereza.
Ligi za Uingereza huenda zikawa miongoni mwa mashindano ya mpira wa miguu ambayo inatumia teknolojia ya picha jongefu ili kuwa na uhakika wa tukio lililotokea muda mfupi uliopita wakati wa mchezo. Teknolojia hiyo tayari inatumika kwenye ligi kuu ya Italia na Uhispania.
Majaribio yatafanyika katika jumla ya mechi kumi na mitanno (15) baada ya mapumziko kutoka mechi za kimataifa kwa timu za taifa na kwa mara ya kwanza itatumika Sept. 15 kwenye mechi 5 za saa 9 Alasiri.
Kitendo cha kutumia usaidizi wa picha ya mnato ili kuweza kufanya maamuzi sahihi kitakuwa cha aina yake kwani hakutakuwa na mawasilliano kati ya mwamuzi anayechezesha mchezo uwanjani na wale wengine ambao watakuwa kwenye chumba maalum wakiendesha mfumo mzima wa teknolojia hiyo (VAR).
Kabla ya kuidhushwa kwa kutumiwa kwa teknolojia ya usaidizi wa kufanya maamuzi kupitia picha jongefu kampuni inayoendesha mfumo mzia itapelekea ilichokiona kwa wanahisa wa ligi kuu ya Uingereza kwa ajili kuidhisha rasmi.