Ripoti mpya zaidi kutoka vyombo vya habari vya Korea Kusini vinasema huenda Kampuni ya Samsung ikaondoa sehemu ya kuchomekea spika za masikioni (earphone jack) katika simu zake za matoleo yajayo.
Taarifa hizo zinasema huenda Samsung Galaxy Note 10 ikawa ndio simu ya kwanza kutoka kampuni hiyo kutokuwa na sehemu hiyo. Hakuna sababu zilizotajwa kwanini Samsung inachukua hatua ya kuondoa kitu hicho kwenye simu zake, lakini ripoti inasema kwa familia ya simu za ‘S’ inaweza kusubiri mpaka kufikia toleo la Samsung S11.
Earphone/Headphone jack ni ile sehemu yenye tundu la kuingizia spika za masikioni kwa ajili ya kusikilizia muziki masikioni au kuchomeka Spika kwa usikivu mkubwa zaidi.