Unakumbuka Apple wametoa tundu la spika za masikio katika matoleo yote ya iPhone zake ambazo zinatoka? pengine sasa imefika zamu ya iPad.
Zoezi hili haliishii kwenye iPhone tuu bali linakuja mpaka kwenye vifaa vyake vya iPad na kinachofanyika ni kwamba matoleo yajayo yatakua hayana tundu hilo.
Kwa kuondoa eneo la tundu la spika za masikio ni wazi kuwa jumba la iPad litakua na uwanja mkubwa wa kuongeza baadhi ya vipengele katika iPad zake.
Kumbuka baadhi ya vitu vilivyoondolewa katika jumba la iPhone kuna baadhi ya mambo yaliongezeka kama vile uwezo wa kuongezeka kwa kioo n.k
Vivyo hivyo katika iPad, pengine kuna vitu vingi ambavyo vitaongezeka katika iPad mpya ambazo tunazitegemea kuja.
Lakini ukiachana na hayo hata kwa sasa ni wazi kuwa matumizi ya spika za masikio zenye waya yameshuka sana –sasa watu wanatumia zile amabazo hazina nyanya.
Hata matumizi ya nyaya kwa ujumla yameshuka pia sio? Ndio teknolojia inavyokwenda hivyo bwana ahahaha.
Toleo jipya la iPad linategemewa kutangazwa katika robo ya mwisho ya mwaka huu, pengine haya yote tutayakuta huko……hatuna budi kusubiri.
Sio mara ya kwanza kwa kampuni ya Apple kuja na teknolojia katika vifaa vyake ambavyo kwa namna moja au nyingine inaona kabisa vitakua na manufaa makubwa sana kwa wateja wake…. vile vile mara nyingi wamekua ni watu ambao wanaleta teknolojia mpya katika vifaa
Kingine cha kufurahisha kuhusiana na kampuni ya Apple ni kwamba ukiachana na kampuni hiyo kuwa moja kati ya kampuni zinazojihusisha na teknolojia ambayo ni tajari zaidi lakini bado mara kwa mara wanapambana ili kuhakikisha kuwa wanazidi kushikilia namba za juu kabisa katika soko
Chanzo: The Verge
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika uwanja wa comment, je unadhani ni sahihi kukitoa kipengele hichi cha tundu la spika za masikio katika matoleo mapya ya iPad?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.