Kampuni kongwe inayojihusisha na utengenezaji wa simu za mkoni ya Nokia imetambulisha simu mpya mbili ambazo tayari zimeanza kupokea tathmini chanya kutoka kwa wataalamu mbali mbali wa maswala ya teknologia, simu hizo ambazo ni Nokia Lumia 800 pamoja na Nokia Lumia 710 zote zikiwa zinatumia mfumo wa uendeshaji (Operating System) aina ya Windows Phone uliobuniwa na Kampuni ya Microsoft, Ikiwa ni mara ya kwanza kabisa kwa mfumo huu kutumika kwenye simu za Nokia watumiaji wategemee mabadiliko makubwa na pengine yenye manufaa, katika siku za hivi Karibuni Kampuni ya Nokia imeshindwa kufanya vyema kwenye soko la simu zenye uwezo mkubwa kiteknologia (smart phones) kutokana na ushindani mkubwa kutoka Kampuni nyingine Kama Apple, Samsung, Google pamoja na Blackberry jambo lililopelekea Nokia kuamua kuanzisha uhusiano rasmi na Kampuni ya Microsoft kwa ajili ya kubuni simu zitakazomudu ushindani, tayari kuna tumaini kuwa simu hizi mbili zitafanya vizuri kwenye soko na hii ni dalili nzuri kuwa ushirikiano wa Nokia na Microsoft unaweza kuleta mapinduzi kwenye Teknologia ya simu za Mkononi.
Ili kupata tathmini ya kina juu ya uwezo na ubora wa simu hizo mpya yaani Nokia Lumia 800 na Nokia Lumia 710 endelea kutembelea blog hii.
No Comment! Be the first one.