Ripoti ya robo ya pili ya mwaka huu iliyotolewa na TCRA inatoa picha nzuri juu ya gharama na ukuaji wa huduma za mitandao ya simu. Ripoti hiyo ya mwisho wa mwezi wa sita mwaka huu inakupa picha ya mtandao gani wa simu ni nafuu zaidi, na pia ukuaji wa mitandao hiyo.
Tuanze na ukuaji;
Mtandao wa Halotel na Airtel ndio wamekuwa kwa kasi zaidi katika miezi ya tano na sita mwaka huu kuliko mtandao mwingine wowote wa simu. Wakati Halotel walipata wateja wapya 218,588, Airtel walipata wateja 136,862, wakati Tigo walipata wateja 113,703 na huku Vodacom wakipoteza wateja 5,673 (yaani hawakuwa na ukuaji kabisa).
Data za ukuaji wa wateja wapya.

Je mtandao gani ni nafuu zaidi?
- Gharama za maongezi – simu za maongezi


Gharama za SMS (UJumbe mfupi)
- SMS za ndani ya nchi

- SMS kwenda nje ya nchi

Soko la huduma za kibenki za mitandao ya simu kufikia Juni 2017;

Kwa ufupi;
- Mtandao wa Tigo ingawa ni maarufu sana umekuwa ni mmoja wa mtandao wenye gharama za juu sana. Ila unaonekana unaendelea kukua (umeshikilia nafasi ya tatu)
- Halotel na Airtel wanaukuaji wa mzuri. Inaonekana nguvu ya ziada waliyoweka Halotel kuyafikia maeneo mengi mapya inaonekana kuwalipa – wameendelea kuwa na ukuaji mzuri kwa muda mrefu sasa.
- Kwa ujumla wake mitandao yenye gharama nafuu zaidi ata kama mtumiaji hatumii kifurushi ni Halotel, TTCL, Smart (Benson) na Zantel.
- Airtel Money inaongeza kwa ukuaji ukilinganisha na huduma zingine za kibenki za mitandao ya simu, idadi ya watumiaji ilikuwa kwa asilimia 12 katika kipindi hicho. Ukuaji wake na ule wa TIgo Pesa unaonekana kupunguza idadi ya watumiaji wa M-pesa (Vodacom).